Thursday, September 6, 2012

Wanahabari watembelea taasisi ya utafiti wa zao la Kahawa TACRI mkoani Kilimanjaro

Inatoka http://kilimanjaro-yetu.blogspot.se
Mtafiti katika taasisi ya utafiti wa zao la Kahawa Tanzania,TaCRI
kanda ya kaskazini ,John Mabagala akiwaelezea wanahabari kutoka mkoa

wa Kagera aina mpya za miche ya Kahawa ililiyo fanyiwa utafiti katika

kituo hicho.

Meneja wa programu ya uongezaji tija wa ubora wa Kahawa na msimamizi
wa maabara ya udongo TaCRI,Godsteven Maro akiwalelezea wanahabari jinsi maabara hiyo inavyo fanya shughuli zake.

Mtafiti katika taasisi ya utafiti wa zao la Kahawa Tanzania,TaCRI
kanda ya kaskazini,John Mabagala akizungumza na wanahabari kutoka

mkoa wa Kagera waliotembelea Taasisi hiyo kujionea jinsi inavyo fanya

shughuli zake.zira hiyo iliandaliwa na muungano wa vilabu nchini UTPC
na kuratibiwa na klabu ya wanahabari mkoa wa Kilimanjaro,MECKI.

Waahabari kutoka Mkoani Kagera wakiendelea kutembelea taasisi ya utafiti wa zao la Kahawa nchini TaCRI kujionea shughuli mbalimbali zinzofanywa na taasisi hiyo.

Na Dixon Busagaga waglobu ya jamii Moshi.


WANAHABARI sita kutoka klabu ya wandishi wa habari mkoa wa
Kagera(KPC)wametembelea taasisi ya utafiti wa zao la Kahawa nchini

TaCRI kujionea shughuli mbalimbali zinzofanywa na taasisi hiyo.



Ziara hiyo iliyoandaliwa na muungano wa klabu za waandishi wa habari
nchini(UTPC) na kuaratibiwa na klabu ya waandishi wa habari mkoa wa

Kilimanjaro MECKI ilikuwa na lengo la mafunzo kwa wanahabari kujifunza
na namna gani waandishi wa mikoa mingine wanavyo fanya shughuli zao
ikiwa ni pamoja na jinsi wanavyoshirikiana na wadau.



Wakiwa katika taasisi hiyo ,wanahabari hao walipata maelezo kutoka kwa
Mtafitio John Mabagala kuhusiana na shughuli zinazofanywa na kituo

hicho na baadae walipata fulsa ya kutembelea maeneo mbalimbali kituoni
hapo ikiwemo Maabara ya Udongo,Vitalu vya miche ya Kahawa na maktaba
ya taasisi hiyo.